Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho - podcast cover

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

RFI Kiswahiliwww.rfi.fr

Ni Makala yanayoangazia kwa jicho la tatu mazingira halisi ya dunia yalivyo bila kusahau kile ambacho kinachangia kuyaharibu. Utapata kufahamu namna ambavyo mazingira na rasilimali zinavyoharibiwa huku pia teknolojia ikijumuishwa. Hakika mazingira mazuri ya leo ni dunia yako kesho.

Last refreshed:
Follow this podcast in the Metacast mobile app to refresh it and see new episodes.
Download Metacast podcast app
Podcasts are better in Metacast mobile app
Don't just listen to podcasts. Learn from them with transcripts, summaries, and chapters for every episode. Skim, search, and bookmark insights. Learn more

Episodes

Mradi wa EACOP umekamilika asilimia 62, wanaharakati wakiendelea kuupinga

Ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Uganda kwenda Tanzania maarufu EACOP umefikia asilimia 62, hivi majuzi raia 26 wa Uganda ambao ni waathriwa wa miradi ya mafuta ya Total ya Tilenga na EACOP wamewasilisha keshi mpya dhidi ya kamuni ya TotalEnergies nchini Ufaransa,

Jul 14, 202510 min

Matumizi ya viuatilifu au viuadudu na madhara kwa mazingira

Hatua ya serikali ya Kenya kuoiga marufuku matumizi ya takriban viuatilifu au dawa za kuua wadudu takriban 77 kutokana na hofu ya usalama wa dawa hizo kwa mazingira na afya ya binadamu. Baadhi ya viuatilifu vimepigwa marufuku katika soko la kimataifa, kuanzia baranai ulaya, Australia, marekani na Canada, laini viipo kwenye masoko ya nchi za ukanda.

Jul 01, 202510 min

Vitabu: Kampeni ya kuwafikia watoto milioni moja kuhusu uhifadhi

Watoto wana jukumu muhimu katika uhifadhi wa mazingira na wanyamapori kwa kushiriki kikamilifu katika mipango kama vile kupanda miti, udhibiti wa taka, na kuongeza uelewa kuhusu masuala ya mazingira na wanyamapori. Kuwashirikisha watoto katika shughuli hizi kunakuza hisia ya uwakili, kuwaunganisha na mazingira wanayoishi, na kukuza mazoea endelevu kwa siku zijazo.

Jun 23, 202510 min

Mgogoro wa Bahari: Afrika yataka kushirikishwa kikamilifu katika ulinzi wa bahari

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia kutekeleza lengo nambari 14 la Maendeleo Endelevu, ulifanyika kule Nice, Ufaransa, kujadili mbinu mwafaka za kuhifadhi na kutumia kwa njia endelevu bahari na rasilimali zake, washikadau wakiunda uhusiano mpya kati ya wanadamu na mazingira ya baharini. Mkutano wa kilele ulikamilika Ijumaa tarehe 13 Juni, 2025 wakati huu mataifa yakitarajiwa kukutana mwezi ujao kujadili sheria za uchimbaji madini kwenye kina kirefu cha maji baharini....

Jun 19, 202510 min

Je dunia iko katika njia sahihi kutimiza lengo la kumaliza njaa kufikia 2030?

Jumatano ya Mei 28 2025, dunia itaadhimisha siku ya njaa ulimwenguni, siku hii ikilenga kutoa hamasa na kuchochea hatua kuchukuliwa ili kumaliza njaa duniani. Kulingana na ripoti ya kimtaifa ya 2025 kuhusu migogoro ya Chakula, zaidi ya watu milioni 295.3 katika nchi 53 wanakabiliwa na hali mbaya ya ukosefu wa usalama wa chakula.

May 26, 202510 min

Uchakataji wa plastiki katika kuhifadhi mazingira ya bahari na kupata mapato

Jamii za Pwani ya Kenya, zimekumbatia uchakataji wa plastiki kukabili tatizo la uchafuzi utokanao na taka za plastiki ambapo mujibu wa shirika la mazingira la UNEP, kila siku, kiasi sawa cha malori 2,000 ya kuzoa taka yaliyojaa plastiki hutupwa katika bahari, mito, na maziwa ya ulimwengu.

May 15, 202510 min

Juhudi zinazofanywa na wadau kufadhili wakulima wadogo barani Afrika

Wakulima wadogo wanachangia kwa zaidi ya asilimia 70 uzalishaji wa chakula barani Afrika, hii ni kwa mujibu wa Benki ya Maendeleo barani, Afdb, wakati uo huo, lengo nambari mbili ya maendeleo endelevu ikinuia kumaliza njaa na kuihakikishia dunia usalama wa chakula kufikia mwaka wa 2030

Mar 28, 202510 min

Siku ya wanayampori: Jinsi binadamu hutegemea rasilimali za wanyamapori na bayoanuwai.

Binadamu hutegemea rasilimali za wanyamapori na bayoanuwai ili kukidhi mahitaji yao. Tunahitaji chakula, mafuta, makazi, na hata mavazi. Hivyo ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kwamba mifumo ikolojia inaweza kustawi na mimea na wanyama wanaweza kuwepo kwa ajili ya vizazi vijavyo. Machi 3 mwaka huu, ilikuwa ni fursa ya kutoa uhamasisho wa umuhimu wa wanyama na mimea pori, ili kuongeza ufahamu wa faida zao, na haja ya kuongeza mapambano ya uhalifu dhidi ya wanyamapori na kusababisha athari kubwa...

Mar 11, 202510 min

Utupaji salama wa taka za kieletroniki, mashirika yachangamkia fursa kuokoa mazingira

Taka za kieletroniki zinajumuisha vitu vingi ambavyo ni hatari kwa afya ya binadamu na mazingira na utupaji ovyo ni chanzo kikuu cha madhara, dutu hizi hatari zikiwa na uwezo wa kuchafua udongo, maji, hewa na vyanzo vya chakula. Shirika la E-Waste Initiative Kenya linatoa suluhu ya taka za kieletroniki. Bonyeza hapa kufahamu zaidi.

Mar 04, 202510 min

Mwali wa mwisho: Mkaa wa Briketi kama suluhu ya nishati jadidifu

Mkaa wa Briketi hutengenezwa kutoka kwa vumbi la mkaa wa kawaida, taka za kilimo au mabaki ya mbao, na hutumiwa kimsingi kwa mapishi nyumbani, shuleni na hata katika makampuni. Mkaa huu una faida kwa kuwa unapunguza uchafuzi wa mazingira, kupunguza ukataji wa miti lakini pia huwaka kwa muda mrefu na kwa usawa zaidi kuliko mkaa wa kawaida, na kuufanya kuwa chaguo maarufu kwa kupikia.

Feb 20, 202510 min

Umuhimu wa matumizi ya madawa ya kiasili kunyunyuzia mimea shambani

Makala haya yanazungumzia jinsi Wakulima wengi nchini Kenya wanakumbatia mbinu mpya za kudhibiti wadudu waharibifu wa mimea kwa kutumia madawa ya kiasili badala ya kemikali za viwandani. Kutokana na madhara yanayotokana na matumizi ya dawa za kemikali,wakulima hawa sasa wanageukia madawa hayo asilia kuimarisha mazao na mazingira , Mimea kama vile ,pareto,kitunguu saumu,pilipili na hata mtunguja pori yaani sodom apple sasa inatumika kutengeneza madawa hayo.

Feb 10, 202510 min

Wakaaji wa mijini wanavyotumia Bustani ya Nyumbani kukabili mabadiliko ya tabia nchi

Utunzaji wa bustani ya nyumbani, ni mbinu mpya ya kilimo inayolenga kutimiza malengo matatu kwa wakati mmoja: kuongeza mapato ya kilimo, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuimarisha ustahimilivu, halkadhalika kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi. Bustani ya Nyumbani, kwa kawaida huwa karibu na jikoni au pia kwenye roshani. Bustani hii ambayo mara nyingi hutumia mbolea asilia husaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi kwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafu na pia kutunza udongo. Bus...

Feb 03, 202510 min

Hatua ya Marekani kujiondoa kwa mkataba wa Paris kuathiri nchi maskini

Rais Donald Trump kwa mara nyingine alitangaza Marekani kujiondoa kwenye Mkataba wa Paris kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, hatua ambayo imeibua mjadala wa kimataifa. Tangazo hilo lilikuja huku ulimwengu ukishuhudia viwango vya joto vinavyovunja rekodi na majanga yanayozidi kuwa makali yanayohusiana na hali ya hewa. Lakini wadadisi wa mambo na viongozi wengine wa ulimwengu wanatazamaje hatua yake Trump? Bonyeza usikilize zaidi.

Jan 28, 202510 min

Kenya: Jinsi nguo za mitumba zinachangia katika uharibifu wa mazingira

Sekta ya mitumba inauwezo wa kuchangia mabilioni ya fedha katika mapato ya taifa, pamoja na kutoa maelfu ya ajira katika mataifa ya bara Afrika na ulaya. Kulinga na utafiti wa Oxford Econimics mwaka uliopita; 2024, sekta ya mitumba pekee ina dhamani ya dola bilioni 8 na imetoa ajiri ya idadi ya zaidi laki moja na elfu 60 kwa vijana nchini Msumbiji , Ghana na Kenya . Lakini hata hivyo wanaharakati wa mazingira wanasema baadhi ya nguo hizo za mitumba zinazoletwa Afrika zinachangia katika uchafuzi ...

Jan 23, 202515 min
For the best experience, listen in Metacast app for iOS or Android